Wednesday, November 2, 2011

BREAKING NEWZ: POLISI WALIPUA MABOMU KUTAWANYA WAANDAMANAJI KESI YA KUCHOMA KURAN MWANZA.

Katika hali isiyotarajiwa, ghafla mazingira ya mahakama ya mwanzo iliyoko karibu na ofisi za idara ya maji safi na maji taka jijini Mwanza, eneo la Kemondo na maeneo ya Ghandh hall, Polisi wamelazimika kulipua mabomu ya machozi majira ya saa nne asubuhi ili kuwatawanya waandamanaji waliofurika kwa wingi nje ya mahakama wakifanya vurugu kushinikiza maamuzi yafanyike dhidi ya watuhumiwa wa kesi hiyo….

Jumla ya watuhumiwa wanne wanadaiwa kushirikiana kuchoma Korani, asubuhi ya leo wamefikishwa mahakamani hapa kujibu mashtaka dhidi yao katika kesi inayotajwa kuahirishwa zaidi ya mara nne sasa kutokana na kuhofia usalama wa watuhumiwa.

Watuhumiwa wanaohusishwa na kesi hiyo ni waumini wa Kanisa la Tanzania Assembly of God (TAG) ni Tumaini Jumanne (30) ambaye ni mwalimu wa Biblia, Petro Mashauri (29) mfanyabiashara, Dickson Magai (30) mfanyabiashara na mwanamke pekee, Kalista Mlomo ambaye ni mkulima.

Wakikabiliwa na mashitaka matano ambayo ni kula njama, kufanya kusanyiko lisilo halali, kuingia kwa jinai nyumbani kwa Husna Hamis na kuharibu mali, pamoja na lile linalozungumzwa zaidi la kudhalilisha dini kwa kuchoma moto kitabu cha Korani Tukufu.


Kesi imesababisha barabara kufungwa kwa muda hadi hali itakapo tulia.

Si biashara tena bali msaada kukosha macho kwa maji ya kahawa.

Askari wa jeshi la polisi wakifanya doria eneo la mahakama.

Kutokana na hatua ya kufunga barabara watu wamelazimika kutembea kwa miguu nao polisi wakipiga marufuku kusanyiko la aina yoyote kwenye eneo husika.

No comments:

Post a Comment