Monday, November 7, 2011

John Lisu Amwadhimisha Bwana jijini Mwanza


Mungu ni Roho Nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika ROHO na kweli, Jumapili ya Jana katika ukumbi wa GOLD CREST jijini Mwanza, Mtumishi wa Mungu John Lisu alikuwa akifanya Tamasha la Muziki wa Injili.

KatikaTamasha hilo lililopewa jina la JEHOVA Yu Hai Tour Lisu aliongozana na Timu ya Wapiga Vyombo na waimbaji kutoka jijini Dar.

Kwa yeyote ambaye alifika katika Tamasha hilo atakubaliana nasi kuwa kuna namna ambayo MUNGU anaitembelea Tanzania kwa namna ya Pekee kupitia uimbaji. Safari ya John Lisu katika jiji la Mwanza ilianza kwa Kufanya Tamasha la Kusifu na Kuabudu katika Chuo cha Saint Augustine Univ Siku ya Jumamosi ambapo kwa namna ya Pekee wanachuo walimpokea YESU kama Bwana na Mwokozi wa Maisha Yao, huku John Lisu na watumishi wengine walifanya Maombezi kwa wanafunzi waliokuwa wakisumbuliwa na maradhi mbalimbali.

Katika Ukumbi Gold Crest Tofauti na ilivyozoeleka katika matamasha Mengi kwa wakazi wa Mwanza kukaa na Kumshangaa/ kumwangalia Muimbaji jana ilikuwa Tofauti ambapo kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa Tamasha ilikuwani Two way Traffic Waimbaji waliimba huku pia Hadhira nayo ilimuadhimisha JEHOVA JIRE

Glory To GOD
Yesu Umejivika Haakiiii, na Heshima aaahhh John Lisu akimwamtukuza Mungu jijini Mwanza
.
Askofu Eugine Mlisa mmiliki wa ALIVE Fm akiwafanyia maombi watu wenye uhitaji mbali mbali

John lisu akimtambulisha Mkewe Nelly Lisu kwa wapendwa wa jijini Mwanza


With keyboard anaitwa Prince Adolph Nzwalla Kutoka Hosanna Praise Team pia ni Mtangazaji wa Alive Fm ya Jijini Mwanza ni Moja kati ya Watu waliofanikisha Kufanyika kwa Tamasha la Jehova Yu Hai Tour jijini Mwanza

Sehemu ya Team ya wapiga Vyombo wa Lisu aliofika nao Mwanza kuhudumu

Utukufu Kwa Mungu

Sehemu ya Umati ukimtukuza Mungu ukumbini hapo

Yu Hai Jehovaaa, Yu Hai Mileeelee…….

Ma-back benchers wakipeleka Nderemo Mbele za Mungu

No comments:

Post a Comment